Friday, November 06, 2009

Mengi's Press Conference

Leo Mzee Mengi kakutana na waandishi wa habari (dakika chache zilizopita) na hiki ndicho alichoongea:

TAARIFA YA MWENYEKITI MTENDAJI WA IPP LTD. BW. REGINALD A. MENGI KWA VYOMBO VYA HABARI
6 NOVEMBA, 2009

_____________________________________________


Ndugu Waandishi wa habari,

Nimewaita hapa leo kuzungumza nanyi kwa lengo la kuweka rekodi sawa.

Kwa muda mrefu sasa nimekuwa nikituhumiwa na baadhi ya viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwamba mimi si Mwanachama wa Chama hicho na kwamba sitoi misaada ya hali na mali kwa Chama Cha Mapinduzi.

Ndugu Wanahabari,

Kwa msemo wa kiingereza “Don’t argue with a fool because people may not know the difference between you and the fool”, wenye maana kwamba usibishane na mjinga kwa sababu watu wanaweza kushindwa kufahamu tofauti yako na huyo mjinga!

Hata hivyo wakati mwingine inakulazimu kujibu hoja unapomwona mtu anapotosha mambo kwa makusudi.

Kwanza, kuhusu kuropoka kwamba sitoi misaada kwa CCM, hilo ni jambo linalozushwa na watu binafsi na kwa malengo binafsi. Viongozi wakuu wa CCM ambao ni waadilifu na wanaosimamia ukweli wanajua undani wa jambo hili.

Pili, kuhusu uwanachama wangu wa CCM:

Napenda kuwaambia kwamba mimi ni Mwanachama wa CCM tangu tarehe 18 Aprili,1977 na kadi yangu ni Na. B124595, iliyotolewa na Tawi la Kisutu, Wilaya ya Ilala, Mkoa wa Dar es Salaam.

Hivyo basi madai yote kwamba mimi si mwanachama au nilijiunga na chama hivi majuzi kama inavyoelezwa na Mheshimiwa Waziri wa Utawala Bora Sophia Simba, Katibu wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam, Shaaban Kilumbe Ng’enda na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa DSM John Guninita ni uongo, uzushi na umbea wenye lengo la kudhoofisha juhudi za viongozi wa juu wa CCM na baadhi ya wanachama za kupiga ufisadi vita.

Mimi na wenzangu wengine tumekuwa mstari wa mbele kuhakikisha kwamba chama chetu kinaongozwa katika misingi yake ya asili ya kupiga vita rushwa na maovu mengine.

Ndugu Wanahabari,

Hawa wanaodai kuwa ndani ya CCM hakuna kiongozi msafi ni wazi kwamba wamedandia chama hiki hivi majuzi. Ningetoa ushauri kuwa waondoke na watuachie chama chetu kwa kuwa hawafahamu msingi imara wa CCM.

Mwisho napenda kumshauri Waziri Sophia Simba kwamba katika vita dhidi ya ufisadi ni vyema akanyamaza. Kwa sababu yeye si mwadilifu na hivyo hawezi kusimama kupinga vita ya ufisadi.

Aidha, ningemshauri kabla hajazungumza aombe ushauri kutoka taasisi za serikali kama vile usalama wa taifa badala ya kuropoka na kupotosha ukweli wa mambo.

Nawashukuru sana kwa kunisikiliza.


Reginald A. Mengi

MWENYEKITI MTENDAJI, IPP LTD.
__________________

Thursday, November 05, 2009

Kipanya leo

Wednesday, November 04, 2009

Day 58 on M-Net’s Big Brother Revolution


Day 58 on M-Net’s Big Brother Revolution and the housemates welcome a new addition to the house, as “man’s best friend” Ruby makes her appearance. Meanwhile the housemates have been given the formidable task of creating a new garden for the Big Brother house and have been busy planting, watering and digging! And the tension grows as the days pass and another eviction looms ever closer! Tune in to Big Brother Revolution on DStv channel 198 or 199 and for more information, log on to www.mnetafrica.com/bigbrother.

Tuesday, November 03, 2009

Vodacom Miss Tanzania Miriam Gerald


Vodacom Miss Tanzania Miriam Gerald akiwapungia mkono akiwa ndani ya gari lake lililosajiliwa kabisa baada ya kukabidhiwa jana na wadhamini wakuu wa mashindano ya Miss Tanzania, Kampuni ya Vodacom Tanzania na washirika wake wa huduma, Shivacom jana. Gari hilo lina thamani ya sh. 53.2 milioni. (Picha/Majuto Omary)

Sitta na Hosea uso kwa uso


Mkurugenzi Mkuu wa PCCB, Dr. Edward Hosea, amemtembelea Spika wa Jamhuri ya muungano Mh. Samuel Sitta Bungeni leo Dodoma. Pichani Spika akimkaribisha Hosea mara baada ya kuwasili ofisi za Bunge. Kulia ni Mheshimwia Nyalandu

JK aifariji familia ya Ng'itu



Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisaini kitabu cha maombolezo nyumbani kwa aliyekuwa mbunge wa Ruangwa CCM marehemu Sigfrid Ng'itu wakati Rais Kikwete alipokwenda nyumbani kwa marehemu Mbezi beach Dar es Salaam kuifariji familia yake.Marehemu Ng'itu alifariki usiku wa kuamkia leo katika hospitali ya taifa Muhimbili alikokuwa amelazwa tangu Septemba 15 mwaka huu akisumbuliwa na ugonjwa wa kiharusi.

Binti wa miaka 11 ajifungua mtoto siku ya harusi


SOPHIA, BULGARIA
Msichana mdogo mwenye umri wa miaka 11 kutoka nchini Bulgaria wiki iliyopita alijikuta akiwa mama baada ya kujifungua mtoto wake siku ya sherehe ya ndoa yake na kijana mdogo mwenye umri wa miaka 19 ambaye ni baba wa mtoto huyo.
Kordeza Zhelyazkova alikuwa bado amevalia gauni lake la harusi pamoja na taji yake wakati akiwasili hospitalini na kujifungua mtoto wa kike aliyempa jina la Violeta.
Msichana huyo alijihisi kuwa ana mimba wiki mbili baada ya sikukuu yake ya kuzaliwa. Alijifungua wiki iliyopita akiwa na mumewe pembeni aliyejitambulisha kwa jina la Jeliazko Dimitron.
Kordeza alijifungua salama mtoto wa kike mwenye uzito wa kilo 2.4 ambaye alimpa jina la Violeta lakini alitoroka hospitali na mtoto wake usiku huo huo aliojifungua mtoto wake ili awahi kumalizia sherehe za harusi yake.
Binti huyo alisema hataki tena kuendelea na shule na anataka atumie muda mwingi kucheza na mtoto wake.
Kordeza ambaye alikuwa ni mwanafunzi wa shule ya msingi, alisema kuwa alikutana na mumewe mpya kwenye viwanja vya michezo vya shule yake baada ya Jeliazko kumuokoa kutoka kwenye kipigo cha wahuni wa mitaani.
Kordeza anadai alianza kufanya mapenzi na Jeliazko bila kutumia kondomu na anakiri alikuwa hajui kondomu ni kitu gani wakati huo.
Kordeza alipata mimba ndani ya wiki moja baada ya kuanza kufanya mapenzi na mpenzi wake huyo.

Muhimbili sasa imebadilika




HOSPITALI ya Taifa Muhimbili inafanyiwa mabadiliko makubwa hebu cheki hapa reception pamoja na jengo la Chuo kikuu cha Muhimbili, kwa kweli ipo hatua kubwa suala ni kwamba je tutaweza kumaintain standard ya juu kiasi hiki.Jana Rais Jakaya Kikwete amewataka watanzania kutoenda kutibiwa katika hospitali ya Taifa Muhimbili wakitokea majumbani mwao bali waende baada ya kupata rufaa za hospitali za wilaya na rufaa.
Rais alitoa kauli hiyo jana wakati waziara yake iliyoambatana na ufunguzi wa kitengo cha matibabu ya Figo.
“Muhimbili inapaswa kuwa ni hospitali ya kutibu magonjwa makubwa yanayoweza kupelekwa nje ya nchi,lakini magonjwa ya kawaida yanapaswa kutibiwa katika hospitali ya Wilaya pamoja na Zahanati”alisema Rais Kikwete na kuongeza:
“Hii ni hospitali ya rufaa inayopokea wagonjwa kutoka hospitali zingine si kila mgonjwa anapaswa kutibiwa hapa wengine watibiwe kwenye hospitali zilizoko jirani na maeneo wanakoishi wagonjwa”.
Rais pia lisema kuwa lengo la serikali ni kuwapatia wananchi huduma bora ya afya na ndiyo maana hivi sasa kuna sera ya kuijenga vituo vya afya na zahanati jirani na makazi ya wananchi.
Kuhusu hatua ya watanzania kwenda kutafuta matibabu ya nje ya nchi Rais Kikwete alisema serikali inaendelea kufanya jitihada za kuboresha huduma ya afya nchi ili wananchi wasiende kutibiwa nje ya nchi.
“Hakuna haja ya watanzania kwenda kutibiwa nje ya nchi kwa sababu hivi sasa tunajitahidi kuboresha huduma ya afya nchini kadri ya uwezo wetu katika hospitali hii ya muhimbili”:
“Nimeelezwa kuwa hivi sasa kunakitengo cha matibabu ya Figo hapa Muhimbili hivyo watu wanaohitaji kubadilisha damu watapa huduma hiyo hapa hakuna haja ya kwenda Kenya au India kwa ajili ya kubadilisha damu”alifafanua Rais Kikwete.
Aliongeza kuwa “Hapo nje tumeonyeshwa ramani ya majengo mawili makubwa yanayojengwa na wachina yatakapo kamilika yatatumika kwa ajili ya upasuaji wa moyo”.
Mbali na ufunguzi wa kitengo hicho cha Figo Rais pia alifungua jengo jipya ya kitengo cha matibabu ya dharura liyofunguliwa na taasisi ya misaada ya kibinadam ya ‘Abbott Fund’.Imeandikwa na Jackson Odoyo.

Monday, November 02, 2009

sare mpya mgambo wa jiji Dar


Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,Willium Lukuvi (wapili kushoto) akikagua gwaride la heshima la Askari wa jiji wakati wa uzinduzi wa sare mpya za Mgambo jijini Dar es Salaam jana. Picha na Venance Nestory

Mbunge Ng'itu afariki dunia


BUNGE la Jamhuri ya Muungano limempoteza mbunge wake wa tisa tangu liingie rasmi mwaka 2005 baada ya Sigifrid Ng’itu, 55, wa Jimbo la Ruangwa mkoani Lindi kufariki dunia juzi usiku akiwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili alikokuwa amelazwa.

Kifo cha mbunge huyo, ambaye alikuwa amelazwa tangu Septemba 14 kwenye Kitengo cha Mifupa (Moi), kililifanya Bunge lilazimike kuahirisha kikao chake cha tano cha mkutano wa 17 hadi leo.

Tangu kuanza kwa Bunge la tisa la Jamhuri ya Muungano, jumla ya wabunge tisa wamekwishapoteza maisha ambao ni pamoja na Salome Mbatia (Viti Maalum, CCM), Amina Chifupa (Viti Maalum, CCM), Chacha Wangwe (Tarime, Chadema), Benedict Losulutya (Kiteto, CCM), na Juma Jamalidini Akukweti (Tunduru, CCM).

Wengine ni Richard Nyaulawa (Mbeya Vijijini, CCM), Faustin Kabuzi Lwilomba (Busanda, CCM) na Phares Kabuye (Biharamulo Magharibi, TLP), ambaye alifariki kwa ajali ya gari wakati akiwa amekata rufaa ya kupinga hukumu iliyobatilisha ubunge wake.

Lakini wakati Bunge likipoteza mtu wa tisa, katibu mkuu wa CCM, Yusuf Makamba, ambaye pia ni mbunge wa kuteuliwa, alitumia msiba huo kuipigia debe CCM ili ishinde katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2010.

Akizungumza na waandishi wa habari katika lango kuu la Bunge, Makamba alisema mbunge huyo alikuwa ni amana kwa CCM, wananchi wa Ruangwa na Tanzania kwa ujumla na hivyo atakumbukwa daima.

“Pengo la jino la dhahabu huzibwa kwa dhahabu hivyo ninaamini wananchi wa jimbo lake hawatafanya makosa katika uchaguzi mkuu wa 2010 na watakichagua Chama Cha Mapinduzi,” alisema Makamba.

Stendi Kuu Ubungo yakabidhiwa kwa serikali



MAkabidhiano ya uendeshaji Kituo cha Mabasi yaendayo mikoani Ubungo (UBT) jijini Dar es Salaam yamefanyika usiku wa manane kuamkia jana ambapo kampuni inayomilikiwa na familia ya Kingunge ilimaliza mkataba wake rasmi na kukabidhi kituo hicho mikononi mwa Serikali.
Huku akikanusha kuwa kampuni ya Smart Holdings Limited iliyoendesha kituo hicho kuhusika na familia ya mwanasiasa Kingunge Ngombale Mwiru, Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo Hassan Khan aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa kampuni yake imemaliza mkataba wake wa miaka mitano ambapo saa sita usiku wa juzi (Jumamosi) ilikabidhi uendeshaji UBT kwa serikali.
"Makabidhiana hayo yalifanyika usiku wa saa sita kwa sababu ya mkataba wetu ulikuwa unaishia tarehe na siku ya 'wikiendi' (Mwisho wa wiki',"alisema Khan na kufafanua kuwa waliokuwepo kwenye makabidhiano hayo ni Mkurugenzi wa Jiji Alhaji Kingobi, uongozi wa jiji wa wakati huo chini ya Wilfred Mukama na utawala wa UBT. Leo watendaji kutoka halmashauri ya jiji wameonekana wakidunda mzigo pasipo utani, wamechachamaa.

Sunday, November 01, 2009

Rais Kikwete Mbeya


Mmmiliki wa kiwanda cha kukata mawe mjini Mbeya cha Marmo Granito Mines Limited Bwana Firoz Jessa akimwonesha Rais Jakaya Mrisho Kikwete aina mbazlimbalzi za mawe ya Marumaru yanayozalishwa na kiwanda hicho wakati Rais kikwete alipotembelea kiwanda hicho kukagua ujenzi unaoendelea na mitambo mbalimbali.Pemebeni nia mke wa rais Mama Salma Kikwete.

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Bia Tanzania TBL Bwana Robin Goetzsche akimwonesha Rais Jakaya Mrisho Kikwete mitambo ya kisasa ya kuzalisha bia muda mfupi baada ya Rais Kikwete kuweka jiwe la msingi katika kiwanda hicho mjini Mbeya leo mchana.Kushoto ni meneja wa kiwanda hicho Bwana Calvin Martin.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akifunua kitambaa kuashiria kuweka jiwe lamsingi katika kiwanda cha Tanzania Breweries Limited (TBL) Tawi la Mbeya leo mchana.Kushoto anayepiga makofi ni Mwenyekiti wa Bodi ya TBL Waziri Mkuu mstaafu David Cleopa Msuya na kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa TBL Bwana Robin Goetzsche.

Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mkoa wa Mbeya Dr.Harun Machibya akimuongoza Rais Jakaya Mrisho Kikwete kukagua baadhi ya majengo ya hospitali hiyo jana muda mfupi baada ya Rai Kuweka jiwe la msingi katika hospitali hiyo leo mchana(picha na Freddy Maro0

PC-Rais Kikwete akishuka kwenye ngazi mara baada ya kuzindua huduma ya gari linalotembea kutoa huduma katika kituo cha afya cha elembo Mbeya vijijini alipodhuru kata hiyo na kuzungumza na wananchi.

Friday, October 30, 2009

Convocation ya Open University


Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na Mkuu wa Chuo Kikuu Huria, k. John Malecela (wapili kushoto) na Makamu Mkuu wa Chuo hicho, Profesa, Tolly Mbwete (kushoto) katika mkutano wa wahitimu wa Chuo Kikuu Huria eneo la Biafra jijini Dar es salaam Oktoba 30, 2009. Kulia ni mkewe Tunu. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)