Sunday, February 24, 2013

JULIET NAIVASHA AJISHINDIA Tsh 5,000,000 KUPITIA DStv REWARDS

Mshindi wa pili wa DStv Rewards, Juliet Naivasha, akifurahia zawadi yake ya kitita cha Tshs Milioni 5 kama inavyoonekana katika mfano wa hundi aliyoishikilia.
Kwa wiki ya pili mfululizo, wateja wa DStv wanaolipia akaunti zao kila mwezi kabla hazijakatwa na hivyo kuingia katika droo maalumu inayochezeshwa kila wiki na kutoa nafasi kwa wateja kujishindia mamilioni ya fedha imeendelea tena kwa kumpata mshindi wake wa pili. Kupitia kampeni hiyo ambayo imepewa jina la DStv Rewards, Juliet Naivasha, mfanyakazi wa National Bank Of Commerce (NBC), amekuwa mshindi wa pili na kujishindia kitita cha Tshs 5,000,000 (Milioni 5).
Mshindi wa pili wa DStv Rewards, Juliet Naivasha ( wa pili kutoka kushoto), akiwa na wafanyakazi wa MultiChoice Tanzania (Ronald Shelukindo na Furaha Samalu) pamoja na Mama yake mzazi, Hilder Lawrence Nyambo (anayemfuatia katika picha) pamoja na mdogo wake Lisa (kulia)
DStv Rewards ni sehemu ya kampeni maalum ya kampuni ya MultiChoice Tanzania kuwashukuru wateja wao kutokana na ushirikiano mkubwa inaoupata kutoka kwao. Akiongelea DStv Rewards, Meneja Masoko wa kampuni ya MultiChoice Tanzania, Furaha Samalu, amesema DStv Rewards ipo wazi kwa kila mteja na hivyo amewashauri waendeleee tu kulipia akaunti zao kabla hazijakatwa ili wapate nafasi ya kuibuka washindi. Wakati huo huo: Mteja wa DStv, Bwana John Komakoma,ameibuka mshindi katika droo nyingine ambayo imepewa jina la Spot The Rewards Box ambapo pindi mteja akiwa anatizama televisheni na kufanikiwa kuona kibox fulani chenye nembo ya DStv, anatakiwa kutuma SMS yenye majina yake yote mawili na namba yake ya simu kwenda katika namba +27 711 745 622 ndani ya dakika tano tangu alipokiona "kibox". 
  
 Kwa ushindi huo Bwana John Komakoma ameshinda Subscription ya mwaka mzima (miezi 12) ya DStv.Kwa maana hiyo, Bw.John ataendelea kufaidi DStv bila malipo yoyote kwa kipindi cha mwaka mzima!
Mshindi wa droo ya Spot The Rewards Box, Bw. John Komakoma (katikati) akipongwezwa na Meneja Uendeshaji wa MultiChoice Tanzania, Baraka R.Shelukindo huku Meneja Masoko wa MultiChoice Tanzania, Furaha Samalu akishuhudia. Bw. John Komakoma amesema yeye ni shabiki wa Liverpool wa kutupwa!Kampuni ya MultiChoice Tanzania kupitia DStv inawapongeza washindi wote.

No comments: