Monday, February 04, 2013

MAADHIMISHO YA MIAKA 36 YA CHAMA CHA MAPINDUZI CCM

Mwenyekiti  wa CCM Taifa, Rais Jakaya Kikwete akihutubia maelfu ya wakazi wa mji wa Kigoma na vitongoji vyake hii leo wakati wa kilele cha maadhimisho ya miaka 36 tangu kuzaliwa kwa CCM.

Pamoja na mamombo Mengine, Rais Kikwete amesema kuwa Chama cha Mapinduzi kitaendelea na jitihada zake za kuisimamia Serikali ili itemize ahadi zake ilizoahidi, huku yeye binafsi akisema kuwa anataka akimaliza muda wake wa uongozi akiache chama hicho kikiwa na heshima na hata Rais ajae atoke ndani ya CCM.

Umati wa wakazi wa Mkoa wa Kigoma.
Mwenyekiti wa CCM, Ndugu Jakaya Kikwete ambaye pia ni Rais wa Tanzania akisalimia watu.
Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harison Mwakyembe akizungumzia mafanikio na mikakati ya sekta ya Usafiri hjasa reli kwa wakazi wa Kigoma.
 Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi, Nape Nnauye akizungumza jukwaani

Furaha ya mmoja wa wakazi wa mji wa Kigoma.
Huu ni ubunifu kwa jirani zetu wa Burundi kwa kulai fimbo za kupigia ngoma.

Kikosi cha Bendera kikipita mbele ya Mgeni rasmi.
Gwaride maalum la Vijana wa Chipkizi lilifanyika mbele ya Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Ndugu Jakaya Kikwete.
Mbunge Catherine Magige na viongozi wengine walikuwepoi uwanjani hapo.
Sura zenye matumaini ya jambo flani
Halaiki iliyo hudhuria
Bango la JK wa wili Jakaya Kikwete na Julius Kambarage
Wanahabari wa vyombo mbalimbali wakiwa kazini.

Kundi la Ngoma kutoka Burundi Mkoa wa Makamba likiburudisha
Msanii wa Bongo Fleva, Nasib Abdul 'Diamond' akitoa burudani uwanjani hapo. PICHA ZOTE NA HABARI ZA MROCKY MROCKY.

No comments: