Saturday, February 16, 2013

Mjumbe wa NEC, Lindi mjini na Mke wa Rais Mama Salma Kikwete Kijiji cha Kineng'ena Kata ya Chakonji na Nanyanje Mkoani Lindi

 Mjumbe wa NEC, Lindi mjini, Mama Salma Kikwete akishiriki kucheza ngoma ya Tambiko Chikonje
 Mjumbe wa NEC, Lindi mjini, Mama Salma Kikwete akiwasalimiana na wananchi kwenye mkutano wake chikonje
Mjumbe wa NEC, Lindi mjini, Mama Salma Kikwete akihutubia mkutano wa hadhara katika Kijiji cha Kineng'ena Kata ya Chakonji akiwa katika ziara ya kuwashukuru wanachama kwa kumchagua u-NEC, kukagua na kuimarisha uhai wa Chama wilaya ya Lindi, Feb 16, 2013.
 Mjumbe wa NEC, Lindi mjini, Mama Salma Kikwete akipokea kadi ya Cuf kutoka kwa mwanachama wa zamani wa chama cha CUF Bahati Athuman baada ya Kuhamia CCM
Mwenyekiti wa Kamati ya miradi ya Maendeleo ya Jamii ya TASAF, katika kijiji cha Nanyenje,  Bakari Kalulu (kulia) akitoa maelezo  kwa wananchi, baada ya Mjumbe wa NEC, Mama Salma Kikwete (kushoto) kumtaka kutoa ufafanuzi kwa nini Ujenzi wa shule ya sekondari ya Kata ulihamishwa kutoka katika kijiji hicho na kupelekwa kijiji kingine cha jirani. Alisema uamuazi huo ulifanywa ili kutoa kipaumbele zaidi kujengwa zahanati.
 Mjumbe wa NEC, Lindi mjini, Mama Salma Kikwete akizungumza na wana ccm kwenye Ofisi ya CCM Chikonje
 Wanachama wapya wa Chikonje Wakila Kiapo
 Wasaniii wa ngoma ya Tambiko Chikonje wakifanya vitu vyao
 Kina mama wa Kijiji cha Kineng'ene wakifuatilia kwa makini hotuba ya Mama Salma alipowahutubia wananchi kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji hicho, akiwa katika ziara ya kuwashukuru wanachama kwa kumchagua u-NEC, kukagua na kuimarisha uhai wa Chama wilaya ya Lindi, Feb 16, 2013.
 Pichaa juu na chini Sura zenye Bashasha zikimsikiliza Mjumbe wa NEC, Lindi mjini, Mama Salma Kikwete
Mjumbe wa NEC, Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akimsalimia Fatuma Mohamed ambaye ni Mama yake mdogo, alipopita katika kijiji cha Nanyanje, akiwa katika ziara ya kuwashukuru wanachama kwa kumchagua u-NEC, kukagua na kuimarisha uhai wa Chama wilaya ya Lindi, Feb 16, 2013. katikati ni Hamis Marobona, mume wa Fatuma.
Mjumbe wa NEC, Mama Salma Kikwete akiwa nyumbani Fatuma Mohammed ambaye ni Mama mdogo wake, alikoamua kumsalimia katika kijiji cha Nanyanje, akiwa katika ziara ya kuwashukuru wanachama kwa kumchagua u-NEC, kukagua na kuimarisha uhai wa Chama wilaya ya Lindi, Feb 16, 2013. Wapili kushoto ni Hamis Marobona, mume wa Fatuma.Picha na Bashir Nkoromo-Idara ya itikadi na Uenezi-CCM

No comments: