Monday, February 04, 2013

MKURUGENZI MKUU WA UNESCO IRINA BOKOVA’S AWASILI NCHINI KWA ZIARA YA KIKAZI YA SIKU MBILI


Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk. Shukuru Kawambwa akimlaki Mkurugenzi Mkuu wa UNESCO Bi. Irina Bokova’s aliyewasili nchini usiku wa kuamkia leo kwa ziara ya kikazi ya siku mbili nchini. Waliobaki nyuma ni Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Tanzania Dkt. Alberic Kacou, Balozi wa Tanzania nchini Ufaransa Mh. Begum Taj na Msaidizi wa Mkurugenzi wa UNESCO.

Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk. Shukuru Kawambwa (kulia) akimwongoza Mkurugenzi Mkuu wa UNESCO Bi. Irina Bokova’s sehemu ya mapumziko kwa viongozi mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwl. Julius Nyerere (VIP Terminal) usiku wa kuamkia leo . Bi. Irina Bokova’s atakuwa nchini kwa ziara ya Kikazi ya siku mbili itakayoanza leo.

Mkurugenzi Mkuu wa UNESCO Bi. Irina Bokova’s akisalimiana na Katibu Mkuu wa Natcom Prof. Elizabeth Kiondo. Wanaoshuhudia tukio hilo Mkurugenzi Msaidizi wa UNESCO Africa Bi. Lalla Aicha Ben Barka (wa pili kushoto) na Mwakilishi wa Shirika la UNESCO nchini Tanzania Vibeke Jensen (kulia).

Mkurugenzi Mkuu wa UNESCO Bi. Irina Bokova’s ( wa pili kulia) akizungumza jambo na mwenyeji wake Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Dk. Shukuru Kawambwa. Kushoto ni Balozi wa Tanzania nchini Ufaransa Mhe. Begum Taj na kulia ni Mwakilishi wa Shirika la UNESCO nchini Tanzania Vibeke Jensen.
Mkurugenzi Mkuu wa UNESCO Bi. Irina Bokova’s akibadilishana mawazo na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Dk. Shukuru Kawamba kwenye chumba cha mapumziko katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwl. Julius Nyerere (VIP Terminal) usiku wa kuamkia leo jijini Dar.

Mkurugenzi Mkuu wa UNESCO Bi. Irina Bokova’s (katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na wenyeji wake Waziri wa Elimu na Maufnzo ya Ufundi Dk. Shukuru Kawambwa (kushoto) na Balozi wa Tanzania nchini Ufaransa Mhe. Begum Taj.
Dk. Shukuru Kawambwa akimsindikiza mgeni wake Mkurugenzi Mkuu wa UNESCO Bi. Irina Bokova’s.
Mkurugenzi Mkuu wa UNESCO Bi. Irina Bokova’s akiondoka katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwl. Julius Nyerere (VIP Terminal) mara baada ya kuwasili nchini Tanzania usiku wa kuamkia leo kwa ziara ya kikazi ya siku mbili.

No comments: